pesayetu
Maambukizi ya Ukimwi Yaongezeka Taita Taveta
July 2022
PesaYetu
article

Share

By David Gikaria

Visa vya maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi vimeonekana kupanda maradufu katika kaunti ya Taita Taveta ikilinganishwa na visa vilivyoripotiwa katika mwaka 2020.

Mratibu wa kaunti hii kuhusu maswala ya ukimwi na magonjwa ya zinaa Charity Mwabili amedokeza kwamba kwa sasa visa 8,875 vya maambukizi ya ugonjwa huo vimeripotiwa katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, miongoni mwa visa hivi 5,414 ikiwa ni vijana walio chini ya umri wa miaka 15.

Haya yanajiri ikizingatiwa kuwa miaka ya hapo awali visa vya Ukimwi miongoni mwa watu kati ya umri was miaka 15 hadi 49 vilipungua. Haya ni kulingana na ripoti ya CDIP ya Taita Taveta. 

Bi Mwabili amesisitiza kwamba wizara ya afya katika kaunti hii kwa ushirikiano na washikadau mbalimbali nchini wanapanga mikakati ya kuwahamasisha vijana kuhusu ukimwi na magonjwa ya zinaa,ikizingatiwa kwamba visa vingi vinavyochipuka vya maambukizi vinawaathiri vijana, hasa kutokana na kutokuwepo kwa miundo mbinu kabambe ya kuwapa vijana elimu ya jamii kuhusu jinsi ya kudhibiti msambao wa ugonjwa huu.

Licha ya hayo, washikadau wamesisitiza kuwa kuna haja ya kutumia kinga kama njia moja kudhiti ugijwa huu hatari. 

Kutumia kinga wakati wa kujamiiana, matumizi salama ya sindano (ikiwa ni pamoja na watu katika kazi fulani, kama wauguzi na wachora ngozi (tattoo)) na kutambuliwa mapema ni hatua zinazosaidia kuzuia maambukizi ya Ukimwi na kuzuia kusambaza virusi kwa watu wengine.

Image: Ujumbe kuhusu ugonjwa wa Ukimwi. Asili: Volunteer Mission

Makala Haya Yamechapishwa na Mwanedu Fm Kwa Ushirikiano Na Code For Africa, Kenya Community Media Network Na Baraza La Vyombo Vya Habari Katoliki (Cameco) Kupitia Msaada Kutoka Ushirikiano Wa Ujerumani Kama Sehemu Ya Mradi Wa Jukumu Letu La Kaunti Yetu.

logo
This site is a project of Code for Africa, the continent’s largest network of civic technology and data journalism labs. All content is released under a Creative Commons attribution Licence 4.0. Reuse it to help empower your own community.

2022 PesaYetu

Stay in touch with us
instagramfacebooktwitterlinkedin